Pakistan inazingatia uwezekano wa kusuluhisha biashara na Urusi kwa rubles au Yuan, Rais wa Jumuiya ya Wafanyabiashara wa Pakistani Zahid Ali Khan aliwaambia waandishi wa habari tarehe 27.
Ali Khan alisema, "Bado tunamaliza biashara kwa dola za Kimarekani, jambo ambalo ni tatizo ...... Tunazingatia kutumia rubles au yuan, lakini suala bado halijaamuliwa hatimaye."
Alisema soko la Pakistan linavutiwa na usambazaji wa bidhaa za Urusi, zikiwemo za kemikali na dawa. Ali Khan alielezea, "Tunaona matarajio makubwa ya maendeleo ya uhusiano wa Urusi na Pakistani. Hasa, bila shaka, (Pakistani inapendezwa na) kemikali za Kirusi, bidhaa za kiufundi, karatasi ...... Tunahitaji dawa. Haya ndiyo masuala ambayo yanafanyiwa kazi."
Mwezi Machi mwaka huu, Islamabad na Moscow ziliripotiwa kufikia makubaliano muhimu ya kibiashara kuhusu masuala kama vile uagizaji wa tani milioni mbili za ngano na gesi. Mwezi Februari, Waziri Mkuu wa wakati huo wa Pakistan Imran Khan alikutana na Rais wa Urusi Vladimir Putin kujadili upanuzi wa uhusiano wa kibiashara baina ya nchi hizo mbili. Wawili hao pia walijadili bomba la gesi la Pakistan Stream ambalo limecheleweshwa kwa muda mrefu, bomba la kilomita 1,100 (maili 683) lililokubaliwa mwaka 2015 kujengwa na makampuni ya Pakistani na Urusi. Mradi huo unafadhiliwa na Moscow na Islamabad na utajengwa na wakandarasi wa Urusi.